Jumamosi, 14 Juni 2014

UTANDAWAZI NA MALEZI



Malezi ni njia ya ukuzaji wa mtoto kwa kutarajiwa kufuata tabia na mwenendo unaostahiki, makuzi na mafunzo.kwa watoto na vijana wanaokua katika jamii husika. Kwa ujumla utandawazi ni hali ya mabadiliko katika nyanja mbalimbali za kimaisha ya mwanadamu kama vile Uchumi, Siasa Jamii na Utamaduni na kuwa katika hali ya mfanano mmoja duniani kote. Mabadiliko haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na kukua na kuenea kwa sayansi na teknolojia ambayo imesambaa kwa kiasi kikubwa sana na kugusa karibu kila sekta ya maisha ya mwanadamu.


1:1 CHANGAMOTO KATIKA MALEZI

Kutokana na kukua na kuenea kwa utandawazi kumeathiri suala zima la malezi na kupelekea watu hasa watoto na vijana kukosa mwelekeo bora wa kimaisha kutokana na kulega kwa wakala wa malezi.

 


1:2 WAKALA WA MALEZI

Wakala wa malezi ni vyombo vinavyofanya kazi kwa niaba ya jamii husika katika kuhakikisha kwamba watoto na vijana wanapata malezi na mafunzo mema yanayoendana na jamii hiyo kama vile heshima, nidhamu, staidi mbalimbali za kimaisha ili waweze kujiandaa na maisha yao ya baadae na kuweza kushiriki katika shughuli mbalimbali za uzalishaji bila kupotoka na mambo mabaya yasiyostahiki katika jamii.

Hapo awali wakala wa malezi walikua ni familia, shule na dini pamoja na jamii yote kwa ujumla. Lakini kutokana na jamii kuzidi kukua na kuongezeka katika masuala ya uzalishaji, biashara na kupelekea kukua kwa miji kumesababisha kuongezeka kwa wakala wengine wa malezi kama vile vyombo vya habari hasa runinga, tovuti na simu za mkononi, magazeti na majarida mbalimbali. Makundi rika ambayo yanatokana na kukua na kuenea kwa sayansi na teknologia nayo yamekua ni miongoni mwa wakala wa malezi.. Hivyo kwa pamoja tunaweza kusema kisosholojia kwamba kuna wakala watano wa malezi ambao ni Familia,Dini ,Shule, Vyombo vya habari pamoja na makundi rika.

Wakala hawa wa malezi kila mmoja ana nafasi yake katika suala zima la kutoa malezi kwa vijana na watoto wa jamii husika. Kutokana na kipaumbele cha jamii hiyo kwa vijana na watoto.

1:3 FAMILIA

Kisosholojia familia ni muunganiko wa Baba, Mama na Watoto pamoja na ndugu wengine wa karibu. Kimsingi familia ndiyo muhimili mkubwa katika jamii yoyote ile. Mtoto anapozaliwa huanza kupata malezi kutoka kwa Baba na Mama yake pamoja na ndugu wengine wanaoizunguka jamii hiyo ili aweze kukua kwa kufuata mila na desturi za kimaisha katika jamii yake. Mtoto hufunzwa mambo muhimu kama vile heshima,Utii, adabu na nidhamu mbele ya wazazi wake na watu wengine nje ya familia yake pia hufundishwa stadi mbalimbali za Kimaisha na kujiingiza katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ndani na nje ya familia.

Takribani miongo mitatu imepita tangu tulipopata mafanikio ya sayansi na teknologia ambayo yamekua ni chachu ya mageuzi katika familia zetu na maisha ya jamii nzima kwa ujumla. Mageuzi haya yameziathiri sana familia zetu katika suala zima la malezi, hi imesababisha baba na mama kuwaacha watoto wao wadogo na kwenda kufanya kazi za Ofisini mbali na nyumbani kwa siku nzima na kuwaacha watoto na walezi wengine..Hapo awali mwanamke ndiye aliyekua mlezi mkubwa wa familia wakati baba alikua anatoka nyumbani na kumuacha mama na kwenda kutafuta riziki kwa ajili ya familia yote. Mabadiliko haya ya baba na mama wote kwenda kutafuta riziki mbali na familia yao yameleta mmomonyoko wa maadili kwa watoto kwa kiasi kikubwa na kupelekea familia nyingi kusambaratika. wazazi wenyewe kwa wenyewe kulaumiana mwishowe tunaona wazazi wanaanza kupeana talaka.

Wazazi kuachana imekua ni jambo la kawaida katika karne hii ya utandawazi ambako kumepelekea athari mbalimbali katika familia kama vile.

i) Watoto kukosa malezi ya wazazi sahihi
ii) Ongezeko la familia za mzazi mmoja
iii) Ndoa za mikataba
iv) Kuongezeka kwa Umasikini katika ngazi ya kaya na Taifa kwa ujumla.

Kutokana na huu utandawazi tumeona wazazi hawawanyonyeshi watoto wao kwa wakati muafaka unaoshauriwa na wataalamu wa afya ili aweze kuendelea na majukumu yake ya kazini alipoajiriwa au kujiajiri. Hii inapelekea watoto na vijana kupoteza uwezo wao wa kufikiri na kushuka kwa kinga na hivyo kupelekea kupatwa na maradhi ya mara kwa mara na kushindwa kuwa wabunifu wanapokua wakubwa.

Na pia kutokana na huu utandawazi wazazi wanaona kua suala la kulea ni sawa na kupoteza muda wao kwani wana majukumu bora na mazuri kwao wao wenyewe na wala sio kwa watoto wao na kuona kwamba kulea ni kupoteza. bora wawe bize makazini. Hii .inachangia watoto kukosa mwongozo wa maisha yao na kushindwa kutatua matatizo yanayowakabili mbele yao na kushindwa kuendeleza vipaji vyao vya asili kwa ajili ya ;.

i) Kutokujua lugha zao za asili
ii) Kushindwa kumiliki miili yao
iii) Kutokufahamu taratibu na sheria za kijamii
iv) Kutojua mila na tamaduni zao
v) Kutokua na huruma kwa ndugu zao
vi) Uvunjifu wa maadili na kupoteza kabisa malengo ya kimaisha.

Utandawazi huu umeweza kusambaratisha familia zetu moja kwa moja ambapo hapo awali mtoto alikua ni mali ya jamiinzima, anaongozwa na kujirekebisha. Huu utandawazi umesababisha watoto kujitegemea na kujilea wenyewe pasipo kujua mwenendo mzima wa maadili ya jamii zao na matokeo yake ni kama vile.

i) Vijana kutosaidiana na kuthaminiana wao wenyewe.
ii) Kukosa umoja na mshikamano kama ndugu wa moja.
iii) Vita vya wenyewe kwa wenyewe ndani ya jamii moja.
vi) Umimi, Udini, Ukabila na Ukanda vimeyatawala maisha yetu

1:4 MAKUNDI RIKA

Rika ni watu ambao wana umri unaokaribiana na kulingana. Kundi rika anaweza kuwa rafiki ,yako jirani yako au hata mwanafunzi mwenzako. Watu wa kundirika wana uwanda mpana wa mazungumzo tofauti na mazungumzo katika familia au jamii kwa ujumla. Makundi rika ya zamani yaliongozwa na mafunzo ya jamii ya jando na unyago. Walifundishwa namna ya kuishi katika hali ya usawa, upendo, uvumilivu na maarifa mbalimbali ili waweze kukabiliana na changamoto za kimaisha pindi watakapokua na familia zao wenyewe ili nao waweze kuwalea watoto wao katika misingi hiyo hiyo yenye tija kubwa katika maisha yao. Kulingana na mabadiliko ya kimaisha yaliyoletwa na utandawazi yameharibu maana halisi ya mafunzo ya jando na unyago kwa vijana katika jamii nyingi za kiafrika ikiwemo Tanzania.

Makundi rika ya sasa hayana mafunzo yoyote ya kimaadili kwa wakubwa na wadogo zao, yametawaliwa na jaziba, hasira, chuki majivuno na dharau kutunushiana misuli mizozo isiyokua na tija kwao, fujo subira imepotea kabisa. Umaarufu ndio ngao ya maisha yao, kudai haki bila kufanya kazi, hawajui wajibu wao sio kwa wao wenyewe kwa familia zao wala kwa jamii zao. Mwelekeo potevu kwa makundi rika haya ni kutokana na utandawazi ambao umepelekea kulega na kupotea kwa mafunzo yetu ya asili ya jando na unyago na kutekwa kwa kiasi kikubwa na tamaduni za kimagharibi hivyo kujishughulisha zaidi na mambo ya kuiga na kushindwa kufanya mambo yao ya ubunifu na kusahau kabisa tamaduni zao katika suala zima la malezi na kujishughulisha na mambo ambayo hayana tija katika maisha yao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni