1. Kuwakubali
na kuwapenda watoto (Appreciation)
Ni
ngumu kabisa kuwa karibu na watoto na kutafuta kukubalika nao pasipo kwanza
kuwakubali. Mawasiliano yako na wao
yanatakiwa kuwa ya kiwango cha juu kuliko yale unayofanya na watu wazima. Kama ni mzazi, tamani au tafuta kuutumia muda
unapokuwa na watoto vizuri. Wape muda na
wewe kadri inavyowezekana.
Shiriki
nao katika baadhi ya yale wanayoyafanya.
Washirikishe pia katika yale unayodhani watapenda kuona ukiyafanya. Usiwaangalie tu au kuwaacha wakutazame
ukifanya. Kumpakata mtoto wakati wa
hadithi ni mfano wa kushiriki nae. Hii
hujenga mahusiano mazuri sana kwao
.
2. Kuwa
tayari kutumia nguvu zetu au nishati yetu ya mwili kwa ajili yao
Watoto
huwa na nishati au nguvu nyingi katika vile wanavyovifanya. Hali kadhalika mtu anayetamani kuwa karibu
nao ni lazima awe tayari kutumia nguvu zake katika kushiriki nao. Mfano, watapenda kukimbizana, watapenda
kuruka, au kutembea haraka na michezo mingine mingi.
3. Kuwa
na hali nzuri ya utu (Sense of humor)
Hali
hii huwafanya watoto kukuona wewe ni sawa nao.
Watoto hupenda sana pale unapokuwa tayari kucheka na kuwa na hisia kama
walizonazo.
Najua
unahitaji muda wa kuwaza juu ya biashara au kazi zako, na watoto nao kwa upande
mwingine wanataka muda ambao hutawaza yalio yako bali yaliyo yao tu.
Mara
nyingine, watoto hufanya vitu vya kuchekesha, tunachotakiwa ni kucheka nao na
sio kuwacheka. Hii itaepusha kuwaumiza
moyo.
4. Uvumilifu
(Patience)
Uvumilivu
ni muhimu sana kwa yeyote anayetaka kuwa karibu na watoto. Watoto hufanya makosa mengi, na pia ni
wataratibu katika kufanya mambo maana ujuzi wao bado ni mdogo. Kwanza ndio wanajifunza kujitawala na kufuata
maelekezo na pia wanahitaji kukumbushwa mara kwa mara. Ni wakati wa kuulizwa maswali mengi na ya
marudio, hata yale yasiyo muafaka.
5. Kuwa
na huruma (Compassion)
Huruma
kwa watoto huambatana na uvumilivu. Mtu
mwenye huruma ni yule anayetambua pale mwenzake anapokuwa na tatizo au uhitaji
na yuko tayari kutoa msaada. Watoto
humwitaji mtu anayewaelewa na kujali mahitaji yao. Vipo vitu ambavyo vyaweza kuonekana vidogo na
vya kawaida kwetu, kumbe kwa watoto ni vikubwa na vyenye kuwaogopesha
sana. Tunategemea huruma na kujali kwako
kutaongezeka hasa kwa wale watoto wenye matatizo au uhitaji mkubwa mfano:
watoto wenye magonjwa ya kudumu, ulemavu au matatizo ya kifamilia.
6. Kuwa
mtu unayekubali mabadiliko (Be flexible)
Watoto
wako tofauti sana na huwezi kuwa tabiri, mara nyingine watataka kitu fulani na
mara hubadilika. Hawana muda wa kufikiri
athari au usumbufu wa kubadilika au kubadilisha maamuzi yao. Kwa sababu ni vigumu kufahamu ni nini
kitajiri kwa mtoto baada ya muda mfupi ujao basi ni lazima tuwe tayari
kubadilika. Pasipo hili basi utakuwa na
wakati mgumu sana kuwa rafiki wa watoto.
7. Kuwa
Mgunduzi (Be creative)
Mtu
mwenye mawazo na fikra za kigunduzi atapata urahisi sana katika kuwa rafiki wa
watoto. Jaribu kuwa mpya kwa watoto kila
mara, sio kila kitu unachofanya kwao kiwe
ni kile kile siku zote. Amsha hamasa yao
kwa vitu, mambo au mawazo mapya mawakati wote.
Watoto hawapendi kufanya kitu fulani kwa njia au mfumo uleule kila
wakati.
8. Kuwa
mtu wa watu na mpenda watu (Be sociable)
Watoto
huwa wanatusoma sana, pale unapojaribu kuwa mwema kwao, kucheka nao na kuwa
karibu nao na wakati hauko hivyo kwa wengine ndani au nje ya familia yako
unawafanya wasikuelewe na taratibu huanza kukuhofu.
Waruhusu
wakuone ukiwa halisi, hususani unapohusiana na wao pamoja na wengine pia.
Wazazi
au mzazi anayependa kujitenga na kuwa mpweke hupata shida sana katika kuwafanya
watoto kuwa karibu nae.
9. Maanisha
na ujitoe kwao (Be committed)
Wakati
unapoamua kufanya kitu na watoto au mtoto, basi maanisha. Usiwe na vitu vingi wakati mmoja. Wape nafasi yao na iwe yao peke yao.
Jitoe
kufanya vema uwezavyo katika kuhakikisha unawajali na kuwafurahisha
watoto. Watoto pia hufurahi sana pale
wanapoona umetoa moyo wako wote kwa ajili yao. Kama umeamua kuanza kitu nao basi
malizia, usikiachie katikati.
Kama
unajua au kuhisi kwamba hutomaanisha katika lile unalolifanya ukiwa nao basi ni
bora uache mpaka pale utakapojiona kuwa utamaanisha.
kuwa karibu na watoto ni jambo muhimu sana maana utafahamu mengi ikiwemo mwenendo wa mtoto ili baadae aishi na jamii vizuri, wazazi na walezi tunapaswa kuwa karibu saana na watoto wetu ili tufahamu miaenendo yao ya hapo baade.
JibuFuta