Faida/Manufaa
ya Kuwa karibu na Watoto:
Watoto
wanaweza kukufanya kuhisi umuhimu fulani na kuhitajika wakati wote na wao. Mara zote hukubali madhaifu yetu na
kuyashangilia yale wanayoyapenda kutoka kwetu.
Ni
watu wa kusamehe kwa urahisi sana, kamwe hawawezi kuficha wanachofikiri au
kukihisi, uwazi wao huu ni faida kwetu ingawa mara nyingine watu wazima wengine
hukasirika. Ukweli ni kwamba uwazi wao
kwetu haumaanishi kutuumiza au kutuumbua.
Ni
faida kubwa kwetu pale tunapoona ukaribu wetu na mtoto au watoto fulani
unabadilisha maisha au tabia zao.
Kupitia jitihada zako watoto wanaweza kujifunza kujitegemea,
ushirikiano, mambo ya afya, kupendana n.k.
Watoto
wa leo wengi wanaishi au kupitia katika familia zenye mazingira magumu sana,
mfano: Familia zenye ulevi, unyanyasani, talaka na kutengana, matatizo ya
kiuchumi. Watoto hawa wanahitaji kutiwa
moyo kuliko wale wenye hali njema.
Utajisikia faraja sana pale utakaposaidia kwa namna moja au nyingine
mtoto mmoja kuifikia hatima yake vema.
Kuwa
karibu na watoto hutuwezesha kubakia ujana hasa katika fikra zetu. Hali ya kuutazama ulimwengu na maisha kama
mtoto anavyotazama hutupa kupunguza au kuondokana na misongo ya mawazo ya
maisha. Tunajikuta tunafurahia kila kitu
kama vile watoto wafanyavyo, hapa tunasema “Yatazame maisha katika jicho la
mtoto”.
Kwa
kuwa karibu na watoto tunapata nafasi ya kutambua vipawa vyetu, hasa vile
vilivyojificha na kuviweka katika utendaji kwa manufaa ya watoto, sisi wenyewe,
na jamii nzima kwa ujumla.
Hata
kama ukaribu na watoto ilikuwa ni ngumu kwako, taratibu utakapojaribu itafukua
upendo wa kweli toka moyoni mwako na mara utatamani kuwa karibu na kujifunza
kutoka kwao.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni